Beki Juma Nyosso amerejea uwanjani tena siku
chache baada ya kufungiwa kucheza soka miaka miwili kutokana na kitendo cha
udhalilishaji dhidi ya nahodha wa Azam FC, John Bocco.
Nyosso amerejea uwanjani akiwa nahodha na
safari hii akiichezea Team Ismail katika tamasha la Kandanda Day lililofanyika
katika Uwanja wa TCC Chang’ombe jijini Dar es Salaam, jana.
Nyosso aliiongoza timu hiyo kuibuka na
ushindi wa mabao 2-0 na tamasha hilo lilifana huku Team Ismail ikilipa kisasi
cha kutandikwa katika tamasha la mwaka jana.
0 COMMENTS:
Post a Comment