Kikosi cha Ruvu Shooting kimeanza kupata
moto kikionyesha kimepania kurejea Ligi Kuu Bara baada ya kuitwanga Lipuli ya
Iringa kwa mabao 4-0.
Shooting wameibuka na ushindi huo mnono leo
kwenye Uwanja wa Mabatini na kujiweka vizuri kuwania kurejea Ligi Kuu Bara.
Bao la kwanza lilipatikana katika dakika ya
28 kupitia Yahaya Tumbo katika dakika ya 28 kabla ya Issa Kandulu kuongeza la
pili kayika dakika ya 56.
Mabao mengine mawili yalifungwa na Tumbo
katika dakika ya 66 kabla ya Rafael Kyara kumaliza kazi katika dakika ya 80.
0 COMMENTS:
Post a Comment