Wachezaji
makinda pia watapata nafasi kubwa ya kuunganishwa katika kikosi cha kwanza.
Kocha Mkuu wa
Simba, Dylan Kerr amesema wachezaji vijana wamekuwa wakionyesha juhudi kubwa
mazoezini.
“Tumekuwa
tukichanganyika na wachezaji vijana, wako ambao wanaonyesha juhudi kubwa na
kweli wana uwezo.
“Lakini
wanahitaji muda zaidi wa mafunzo, pia wanatakiwa kuwa na nidhamu ya kutaka
kufanikiwa,” alisema.
“Lazima
tutawapa nafasi zaidi kama ambavyo unaona wanafanya mazoezi pamoja na wachezaji
wa timu kubwa. Watakaofanya vizuri, nafasi kwao itaongezeka.”
Simba
inaendelea na mazoezi kwa ajili ya Ligi Kuu Bara ambayo ilisimama na sasa
inatarajiwa kuendelea Desemba 12.
0 COMMENTS:
Post a Comment