Yanga sasa
inapaa kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya kujiweka vizuri na Ligi ya Mabingwa
Afrika.
Lengo la Yanga
ni kupata mechi kadhaa za kirafiki ili kujiweka fiti zaidi na Kocha hans van
der Pluijm atapata muda wa kutosha wa maandalizi.
Mkuu wa Kitengo
cha habari cha Yanga, Jerry Muro amesema wataondoka nchini Ijumaa kwa ajili ya
kambi hiyo.
“Tuko katika
maandalizi ya mwisho kwa ajili ya kutafuta mechi za kirafiki ambazo
zitatusaidia kuwa fiti zaidi.
“Mnajua ugumu
wa michuano ya kimataifa, sisi ni wa kimataifa na maandalizi yetu lazima yawe
ya kimataifa,” alijigamba Muro.
Kambi ya Yanga
inatarajia kuwa katika mji wa Johannesburg ambako itaweka kambi inayotarajiwa
kuwa ya zaidi ya siku tano.
0 COMMENTS:
Post a Comment