February 20, 2016



Vikosi vyote vya Yanga na Simba, tayari vimewasili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam tayari kwa mechi yao ya leo.

Lakini wachezaji wa Simba, ambao walitua uwanjani ahapo baada ya Yanga. Hawajaingia kwenye chumba cha kubadilishia nguo ambacho kawaida hutumiwa na Yanga.


Badala yake wameingia kwenye chumba ambacho hutumiwa na waandishi wa habari wakati wa mikutano yao kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Wachezaji wa Simba waliingia kwenye chumba cha waandishi wa habari na mara moja kuanza maandalizi kwa ajili ya mechi hiyo ambayo itaanza hivi punde.

Hivi karibuni, TFF ilitoa adhabu kwa timu zilizotumia vyumba vya waandishi wa habari au kugoma kuingia vyumbani.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic