April 29, 2016


MSEMAJI WA TFF, ALFRED LUCAS MAPUNDA

Kikao cha Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kilichopangwa kufanyika Jumapili, Mei Mosi 2016, kimeahirishwa hadi Jumanne Mei 3, mwaka huu.

Sababu za kuahirisha kikao hicho ni kwamba baadhi ya wajumbe wamepata udhuru hivyo wangeshindwa kuhudhuria kikao hicho kitakachofanyika
jijini Dar es Salaam kupitia mashauri mbalimbali yaliyowasilishwa.  Wafuatao kesi zao sitasikilizwa katika kikao hicho:

  1. (i) John Bocco – Azam FC
  2. (ii) Shomari Kapombe – Azam FC
  3. (iii) Aishi Manula – Azam FC
  4. (iv) Amissi Tambwe – Yanga SC
  5. (v) Donald Ngoma  - Yanga SC
  6. (vi) Paulo Jinga – JKT Rwamkoma FC
  7. (vii) Kipre Tchetche – Azam FC
  8. (viii) Abel Katunda – Transit Camp
  9. (ix) Zephlyn Laurian – JKT Rwamkoma FC
  10. (x) Idrisa Mohamed – JKT Rwamkoma
  11. (xi) DR. Mganaga Kitambi (Daktari) – Coastal Union
  12. (xii) Herry Chibakasa – Friends Rangers
  13. (xiii) Ismail Nkulo – Polisi Dodoma
  14. (xiv) Said Juma – Polisi Dodoma
  15. (xv) Idd Selaman – Polisi Dodoma
  16. (xvi) Edward Amos – Polisi Dodoma
  17. (xvii) Stewart Hall (Kocha)– Azam FC
IMETOLEWA NA MSEMAJI WA TFF, ALFRED LUCAS MAPUNDA 'MAPS'

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic