May 18, 2016


MPIRA UMEKWISHAAAAAAAADk 90+8 Kipa Dida wa Yanga yuko chini anagaagaa baada ya kupigwa jiwe na shabiki aliye nyuma ya lango
Dk 90+7 Anaingia Mwashiuya kuchukua nafasi Msuva
Mwamuzi bado hajaonyesha kibao cha muda wa nyongeza, mzozo unaendelea hapa uwanjani. Haijulikani hata nini kitafuatia, tutaendelea kuwajuza

Sasa ni Dk ya 90
Dk 89, Anaingia Yondani, anatoka Tambwe
Penalti inapigwa hapa, Dida anaokoaaaaaaaaaa
Wapigapicha kutoka Tanzania wako jukwaani wamefuatwa na kuzuiwa kupiga picha
Fujo zimetawala, vurugu uwanjani hadi polisi wameingia
PENAAAAAAT Dk 87,Wanapata penati baada ya Cannavaro kumwangusha mshambuliaji aliyekuwa anaingia langoni

KADI Dk 86 Cannavaro analambwa kadi nyekundu
Dk 85, Ngoma kaumia, anabebwa na kutolewa nje na machela, lakini wanaonekana kumkimbiza harakaharaka, hali inayosababisha mzozo kidogo
Dk 83, Mechi ni ngumu bado, Yanga wanaonekana kuongeza ulinzi zaidi, kingine wanapaswa kujilinda na fauloSasa bado Dk 10 tu, Yanga wanalazimika kuendelea kuweka ulinzi makini zaidi. Kaseke anaonekana kuwa msaada katika ukabaji

Sasa ni Dk 78, mpira bado unaonekana ni mashambulizi ya zamu. Yanga wawe makini na washambuliaji wa Sagrada, wanaonekana kulazimisha kutaka kuingia kwenye boksi. Wakifanikiwa ni rahisi kwao kufunga au kujiangusha

Dk 75, Ngoma anageuka na kupiga shuti vizuri lakini linapaa juu kidogo
Dk 73, Ngoma anatolewa tena kwenda kutibiwa nje, hii ni mara ya nne.
Dk 71, Sagrada wanashambulia zaidi. Sasa wanabadilisha kutoka mipira ya krosi na kupiga ile ya chini wakitaka kupenyeza katikati ya uwanja

Dk 64 sasa, kidogo Yanga wanaendelea kucheza pasi za haraka, ingawa Sagrada pia wanashambulia mara kwa mara. Dida anaonekana kuwa makini zaidi
SUB: DK 60, Pluijm anamtoa Kamusoko anamuingiza Deus Kaseke. Nafikiri ni kuhofia kupata kadi nyekundu, maana baada ya kupewa kadi ya njano, mwamuzi alishamuonya mara moja. Dalili kwamba angecheza faulo nyingine ingekuwa kadi
Dk 58, Ngoma yuko chini, anaonekana kuwapa wakati mgumu sana. Wachezaji Yanga na wale Esperanca wanazozana sana hapa

Dk 53 sasa, mechi inakwenda kwa kasi sana na Yanga bado wanaonekana kuchangamka
Kipindi cha pili kimeanza, Esperanca wanaonekana kuanza kwa kasi wakipania kupata bao la pili. Lakini Yanga nao wanasukuma mashambulizi

HALF TIME:



Dk 42 hadi 44 Yanga walionekana kuamka na kupiga pasi nyingi. Hata hivyo hawakufanya mashambulizi makali sana. Inaonekana wanakuwa makini sana ili wasifungwe bao tena

Dk 41 sasa, mpira unaonekana kubalansi ingawa Yanga wamekuwa wakishambuliwa zaidi
Dida analambwa kadi ya njano, haikuwa sahihi lakini inaonekana baadaye kuna mchezaji wa Yanga atalambwa kadi nyekundu maana mwamuzi anaitengeneza mapema. Dida aliomba kurudishiwa mpira na waokota mpira waliung'ang'ania, mwamuzi kasema alizozana nao.


KADI: Dk 36 hizi, Cannavaro analambwa kadi ya njano, lakini Love alijilegeza kumtafutia msala. Yanga wanalazimika kuwa makini na kadi hizo za njano. Pluijm pia inabidi awaeleze mapumziko au kuzifanyia kazi
BAO
Dk 25, Esperanca wanapata bao kupiria mshambuliaji wao mkongwe Love Kabungula aliyeunganisha krosi baada ya mabeki Yanga kushindwa kuuwahi mpira

 Dk 24, inaonekana wachezaji wa Esperanca wamepania kuwafanya wa Yanga wapanik
-Kamusoko tayari kalambwa kadi ya njano, Yanga inabidi wawe makini kwa kuwa inaonekana wazi mwamuzi kama anatafuta kadi nyekundu

Dida naye anaanguka hapa baada ya kupangua mpira, inaonekana aligongwa. Kama kuna njama hivi ya kutaka kuwaumiza baadhi ya wachezaji au kuwatafutia kadi

Ngoma anaanguka baada ya kufanyiwa madhambi, lakini inaonekana mwamuzi hajali, mechi inaendelea kwa dakika mbili zaidi.

Mechi imeanza kwa kasi sana, Esperanca wanaonekana wamepania kupata bao la mapema ili kuwachanganya Yanga.



2 COMMENTS:

  1. acha ushabiki kwakua mpira hauonyeshwi ndio ututie ndimu...ma repoter wa kibongo kwa kujikomba tu

    ReplyDelete
  2. Nawapongeza sana Yanga kwa kufuzu hata ingawa wamefungwa huko Angola.Mtu kwao,nilikuwa nimelala bila kujua matokeo,ndipo nikakumbuka na kuingia hapa.Nashukuru sana,nadhani Side hapo CCM Mwanza unafurahi pamoja na mashabiki wengine,conges Mramba

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic