June 18, 2016

MOHAMMMED IBRAHIM AKISAINI SIMBA MBELE YA RAIS WA SIMBA, EVANS AVEVA
Kikosi cha Simba tayari kina viungo watano, lakini haijaridhika imeibomoa Mtibwa Sugar baada ya kumsajili kiungo wake mchezeshaji, Mohammed Ibrahim ‘Rasta’.

Timu hiyo, hadi hivi sasa imesajili wachezaji wanne akiwemo Rasta, Muzamir Yassin pia kutoka Mtibwa, Jamal Mnyate na Emmanuel Semwanza wote wa Mwadui FC.

RASTA WAKATI AKIWA MTIBWA
Licha ya kuwasajili nyota hao, Simba bado inaendelea kufanya mazungumzo ya usajili na wachezaji wengine akiwemo kiungo wa Mtibwa, Shiza Kichuya.


Kwa mujibu wa taarifa 'Rasta' amesaini mkataba wa miaka miwili jana mchana.

Moja ya makubaliano ya Rasta na Simba ni kulipwa Sh 250,000 kila Simba inaposhinda yeye akiwa kikosini lakini dau lake la usajili limefichwa kwa sababu maalum.

 “Tulikuwa hatutaki kuona masuala yetu ya usajili yanafanyika kwa uwazi, kwa sababu nusu ya wachezaji tunaowahitaji kwa ajili ya kuwasajili wana mikataba na timu zao.

“Ukiachana na Rasta wachezaji wengine ambao tumemalizana nao ni Yassin, Mnyate na Semwanza. Huyu Rasta kasaini leo (jana) mchana, amesaini mkataba wa miaka miwili kwa sharti la kulipwa Sh 250,000 kama posho yake kila timu inaposhinda,” alisema mmoja wa viongozi wa Kamati ya Usajili ya Simba. 

Alipotafutwa meneja wa mchezaji huyo, Jamal Kasongo kuzungumzia hilo, alikiri taarifa hizo kuwa za kweli Rasta amesaini mkataba wa miaka miwili Simba.

“Nikutoe hofu tu, Mohammed (Rasta) amesaini mkataba leo (jana) hii na hapa ninapoongea na wewe, ndiyo tunamalizana kwa maana ya kusaini mkataba huo wa miaka miwili,” alisema Kasongo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic