July 1, 2016


Kiungo mshambuliaji mpya wa Yanga, Juma Mahadhi amefunguka kuwa yupo tayari kujiunga na TP Mazembe iwapo watampa ofa ya maana huku akisisitiza anajipanga kuisaidia timu yake katika michezo iliyobaki kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Mahadhi  aliyejiunga na Yanga akitokea Coastal Union ya Tanga, alionyesha uwezo mkubwa katika mchezo dhidi ya TP Mazembe, Jumanne ya wiki hii kwenye Uwanja wa Taifa, Dar ambapo alidumu kwa dakika 65 kabla ya kubanwa na misuli iliyosababisha atolewe na nafasi yake kuchukuliwa na Geoffrey Mwashiuya.

Mahadhi alisema kwa sasa anajipanga upya kwa ajili ya kuisadia timu yake katika michezo iliyobakia ya michuano hiyo ambayo ni ya pili kwa ukubwa upande wa ngazi ya klabu Afrika hivyo hataki kuipoteza nafasi hiyo.

“Ishu kubwa ilikuwa ni misuli ilinikamata na kusababisha nishindwe kuendela na mchezo japo awali nilikuwa nacheza kwa hofu sana, nikiogopa kuharibu lakini kadiri muda ulivyozidi kwenda nikawa naona kumbe naweza kufanya kitu kwa ajili ya timu yangu ila bahati mbaya ndiyo hivyo sikuweza kuendelea na mchezo ambao kwetu ulikuwa na umuhimu sana.

“Lakini naamini nitakuwa sawa mapema tu Mungu akipenda kwa sababu malengo yangu nimeyaweka katika michezo iliyosalia.


“Kama Mazembe watakuwa kweli wananihitaji basi nitakuwa tayari kwenda kujiunga nao iwapo wataleta ofa ambayo itakuwa na maslahi mazuri maana mimi ni mchezaji na kazi yangi ni mpira sasa fursa ikitokea lazima niitumie,” alisema Mahadhi. 

SOURCE: CHAMPIONI

1 COMMENTS:

  1. Pole sana dogo Mahadhi, historia inaonesha kuwa Yanga wanajua kuoa tu kuacha hawawezi! Kama unaitaka TP Mazembe subiri baada ya miaka miwili mkataba wako uishe!!!!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic