August 9, 2016


Kiungo mpya wa Simba, Shiza Kichuya (kushoto), jana alionyesha kiwango cha juu wakati Simba ikiitandika AFC Leopard ya Kenya kwa kuichapa mabao 4-0.

Katika mechi hiyo kusherekea miaka 80 ya klabu ya Simba, Kichuya alikuwa mwiba kwa mabeki wa Leopards na kufanya anavyotaka yeye ikiwa ni pamoja na kusaidia kupatikana kwa mabao mawili na yeye kufunga moja.

Swali, Kichuya ambaye amekabidhiwa jezi namba 25, alivyoanza, unafikiri anaweza kuwa mwenye uwezo wa kubeba mikoba ya mshambuliaji Emmanuel Okwi raia wa Uganda.


Okwi alikuwa akivaa namba 25 na alikuwa tegemeo la Simba katika kutengeneza na kufunga mabao. Lakini kwa kasi hiyo ya Kichuya aliyetokea Mtibwa Sugar, unafikiri atavaa viatu vya Okwi? WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI.

7 COMMENTS:

  1. Kama ataendelea kuwa katika ubora alionesha jana...asipolewa sifa za mashabiki...anaeza akawa mrithi wa okwi...ni kijana mzuri mwenye kipaji kikubwa..na ni hadhina kubwa kwa taifa..!!

    ReplyDelete
    Replies
    1. ICHUYA NI MCHEWZAJI MZURI SANA NA KWA HALI HIYO KUPEWA JEZI NO;25 ATAITENDEA HAKI KWANI ANAJUA SANA, VITU VYOTE VYA MPIRA ANAVYO.KINACHOTAKIWA KLABU KUWATUNZA WACHEZAJI HAWA TUACHE UBABAHISHAJI HASA WANAPOTAKA MASLAHI YAO KUBORESHWA.IONGOZI WASIWAGAWE WACHEZAJI HAWA KWANI WOTE BILA KUJALI KALETWA NA NANI PALE NI WETU SOTE.ZAMANI VIONGOZI KAMA KINA BAMCHAWI NA WENGINE WALIKUA WANAJUA SANA KUWALINDA WACHEZAJI KWA NAMNA MOJA NA NYINGINE KIASI WALICHEZA KWA MUDA MREFU.LEO MCHEZAJI ANAHUMIA KATIKA MAZINGIRA YA KUTATANISHA NA HAKIRUDI SIO YULE TENA.WAKIENDA SEHEMU NYINGINE WANACHEZA NA KWAKIWANGO CHA JUU, BADO ATUJIHULIZI KWA NINI INAKUA HIVI? LAZIMA VIONGOZI WAWAJIBIKE KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE MPIRA UNAMAMBO MENGI SANA.

      Delete
  2. Bilashaka yoyoteile amevaaviatu vyaemma okwi

    ReplyDelete
  3. Kichuya kachukua namba 25 baada ya Hassa Kessy naye kuchukua namba 25 yanga....ni tafakari tu

    ReplyDelete
  4. Hakika Kichuya anaitandea Hali No.25 kama alivyokuwa Okwi.na huo Ni Mwanzo tu

    ReplyDelete
  5. Hakika Kichuya anaitendea haki No 25 kama alivyokuwa Okwi na huu Ni mwanzo tu atafanya makubwa zaidi

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic