February 6, 2017




Mshambuliaji wa zamani wa Simba na Sonderjsyke ya Denmark, Emmanuel Okwi ameombwa ajitahidi angalau kupata wastani wa bao moja kila mechi.


Rais wa SC Villa, Ben Immanuel Misagga amemuomba Okwi kukaza kamba na ikiwezekana kufunga mabao.

“Unarudi nyumbani, lakini tunachotaka kikubwa ni mabao. Kama utaweza angalau kila mechi bao moja,” alisema Misagga wakati akimtambulisha Okwi.



Okwi aliamua kuvunja mkataba na Sonderjsyke kwa madai ya kupata nafasi ya kutosha ya kucheza.

Alijiunga na klabu hiyo akitokea Simba aliyopata nayo mafanikio makubwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic