April 23, 2017



Serikali imeipongeza Serengeti Boys kwa ushindi wa mabao 2-1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya Gabon.

Serengeti Boys wameifunga Gabon katika mechi iliyopigwa nchini Morocco ambako timu hiyo imeweka kambi kujiandaa na michuano ya Kombe la Mataifa Afrika litakalofanyika nchini Gabon.

Msemaji wa Serikali Dk, Hassan Abbas amesema serikali inaipongeza timu hiyo ya vijana chini ya miaka 17 kwa ushindi huo.


Serikali inawasisitiza vijana hao kuendelea kupambana wakiwa wamelenga kufanya vizuri na Watanzania na serikali iko nyuma yao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic