April 12, 2017



Uongozi wa Uwanja wa CCM Kirumba, kupitia Meneja wa Uwanja Ndg Steven E. Shija unapenda kutoa taarifa za uharibifu wa Uwanja.

Mechi iliyochezwa Tarehe 10.04.2017, kwenye Uwanja wa CCM Kirumba kati ya Mbao Fc Vs Simba Sc umesababisha uharibifu Mkubwa kwenye Maeneo ya kuingilia Wachezaji, Waamuzi na Geti Namba 4 ambapo walikuwa wamekaa Mashabiki wa Simba


Uharibifu huo umetokana na Mashabiki wa Timu ya Simba Sc kupanda Juu ya maeneo ya Kivuli yaliyojengwa kwenye maeneo yaliyotajwa ( Vyumba vya Kubadirishia Nguo kwa wachezaji, Waamuzi na Geti namba Nne), uharibifu huo umepelekea kushindwa kufunga Milango ya Mbele ambapo ni hatari kwa usalama wa maeneo hayo muhimu

Hivyo uongozi wa Uwanja umeishazitaarifu Mamlaka husika ili zichukue hatua kwa Wanaohusika ili kuhakikisha eneo hilo linatengenezwa mapema kabla ya Mechi ya Toto African Vs Simba Sc Tarehe 15.04.2017 

"We walk the Talk"

Imetolewa:-
Uongozi wa Uwanja wa CCM Kirumba - Mwanza

11.04.2017

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic