May 4, 2017



Anthony Joshua ameeleza kile alichokuwa akizungumza na Wladimir Klitschko ambaye alimshinda katika raundi ya 11.

Joshua alionekana akizungumza jambo wakati akiendelea kuzichapa na  Klitschko  katika raundi ya sita.

Bondia huyo raia wa Uingereza amesema walibadilishana maneno na  Klitschko  wakati wakiendelea kuzichapa.

“Nilimuambia kama utaniachia nipite raundi hii, basi ujue umekwisha. Naye akajibu kwamba ni lazima atanitwanga na kuniagusha,” alisema Joshua.


Joshua alikuwa wa kwanza kumchapa konde  Klitschko  akalamba sakafu katika raundi ya tano. Lakini raia huyo wa Ukraine naye akarejea na kumtwanga Joshua konde katika raundi ya sita lililomlazimisha kwenda chini.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic