Mwili wa marehemu Shose Shalua Fidelis Masao aliyefariki katika ajali aliyokuwemo nahodha wa Simba, Jonas Mkude, utaagwa Alhamisi.
Taarifa kutoka kwa familia ya marehemu imeelezwa kuwa mwili wa marehemu utaagwa Saa 5:00 asubuhi katika hospitali ya Mwananyamala.
Baadaye ibada itafanyika Saa 7:00 mchana na kwa mara nyingine shughuli za mwili kuagwa katika Kanisa la Roma, Magomeni.
Pamoja na hivyo, familia ya marehemu imewashukuru wadau mbalimbali wa klabu ya Simba na wale wapenda mpira waliojitokeza kutoa rambirambi.
0 COMMENTS:
Post a Comment