June 13, 2017


Beki mpya wa Simba, Shomari Kapombe anaamini Simba itafanya vizuri msimu ujao.

Kapombe amesema Simba imeanza kuonyesha kweli inataka kudumisha kikosi chake, hivyo anaamini itafanya vizuri.

“Ukiangalia usajili unaofanyika sasa na kikosi kilichopo, hakuna ubishi kwamba Simba itakuwa na kikosi kizuri.

“Kikosi kizuri maana yake ni kwamba, tuna nafasi ya kufanya vizuri na litakalofuata ni maandalizi mazuri na ushirikiano wa kutosha,” alisema Kapombe ambaye amerejea Simba.


Kapombe amesaini kuichezea Simba kwa mkataba wa miaka miwili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic