June 20, 2017



Wanafamilia 74 wa mpira wa miguu, wamechukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu.

Hadi zoezi hilo linafungwa leo Juni 20, 2017 saa 10.00 jioni wagombea wote wamerejesha ambako kwenye nafasi ya urais, jumla ya wagombea 10 walijitokeza kuomba nafasi hiyo wakati kwenye makamu rais wamejitokeza sita.

Wadau 58 wamejitokeza kuwania nafasi za ujumbe wa kamati ya utendaji katika Katika Kanda mbalimbali. Zoezi la kuchukua na kurejesha fomu kwa mujibu wa Kanuni ya 10, limefanyika kwa siku tano kuanzia Juni 16, 2017 hadi Juni 20, mwaka huu.

Siku ya kwanza ilipoanza tu, Jamal Malinzi alikuwa wa kwanza kuchukua fomu na kurejesha huku akifuatiwa na Imani Madega, Wallace Karia, Fredrick Masolwa, Athumani Nyamlani, Fredrick Mwakalebela, John Kijumbe, Shija Richard, Ally Mayay na Emmanuel Kimbe.

Waliojitokeza kuwania Makamu wa Rais na kurejesha fomu wako Mulamu Ng’hambi, Michael Wambura, Geofrey Nyange, Mtemi Ramadhani, Robert Selasela na Stephen Mwakibolwa.

Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa kufuata Kanda 13 ni kama ifuatavyo:

Kanda Na. 1 Mikoa ya Kagera na Geita;
  1. Soloum Chama
  2. Kaliro Samson
  3. Leopold Mukebezi
  4. Abdallah Mussa

Kanda Na. 2 Mikoa ya Mara na Mwanza;
  1. Vedastus Lufano
  2. Ephraim Majinge
  3. Samwel Daniel
  4. Aaron Nyanda

Kanda Na. 3 Mikoa ya Shinyanga na Simiyu;
  1. Benista Rugora
  2. Mbasha Matutu
  3. Stanslaus Nyongo

Kanda Na. 4 Mikoa ya Arusha na Manyara;
  1. Omari Walii
  2. Sarah Chao
  3. Peter Temu

Kanda Na. 5 Mikoa ya Kigoma na Tabora;
  1. John Kadutu
  2. Issa Bukuku
  3. Abubakar Zebo
  4. Francis Michael

Kanda Na. 6 Mikoa ya Katavi na Rukwa;
  1. Kenneth Pesambili
  2. Baraka Mazengo

Kanda Na. 7 Mikoa ya Mbeya, Songwe na Iringa;
  1. Elias Mwanjala
  2. Cyprian Kuyava
  3. Erick Ambakisye
  4. Abousuphyan Silliah

Kanda Na. 8 Mikoa ya Njombe na Ruvuma;
  1. James Mhagama
  2. Golden Sanga
  3. Vicent Majili
  4. Yono Kevela

Kanda Na. 9 Lindi na Mtwara;
  1. Athuman Kambi
  2. Dunstan Mkundi

Kanda Na. 10 Mikoa ya Dodoma na Singida; 
  1. Hussein Mwamba
  2. Mohamed Aden
  3. Musa Sima
  4. Stewart Masima 
  5. Ally Suru
  6. George Benedict

Kanda Na. 11 Mikoa ya Pwani na Morogoro;
  1. Charles Mwakambaya
  2. Gabriel Makwawe
  3. Francis Ndulane
  4. Hassan Othman ‘Hassanol’ 

Kanda ya 12. Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga
  1. Khalid Mohamed
  2. Goodluck Moshi
  3. Thabit Kandoro

Kanda Na. 13 Mkoa wa Dar es Salaam
  1. Emmanuel Ashery
  2. Ayoub Nyenzi
  3. Saleh Alawi
  4. Shaffih Dauda
  5. Abdul Sauko
  6. Peter Mhinzi
  7. Ally Kamtande
  8. Said Tully
  9. Mussa Kisoky
  10. Lameck Nyambaya
  11. Ramadhani Nassib
  12. Aziz Khalfan
  13. Jamhuri Kihwelo
  14. Saad Kawemba
  15. Bakari Malima

Kwa siku tatu, kuanzia kesho Juni 21 hadi 23, mwaka huu kwa mujibu wa kanuni ya 11.1 ya Uchaguzi wa TFF, Kamati ya Uchaguzi itaanza mchujo wa awali kwa wote waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali kama inavyojionesha hapo juu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic