Pamoja na kuumia kwa beki wa kulia wa Taifa Stars, Shomari Kapombe, kuna matumaini baada ya beki mwingine, Hassan Kessy kuanza matokeo.
Kessy alikuwa akisumbuliwa na misuli lakini amerejea na kuanza mazoezi na kikosi cha Stars jijini Mwanza.
Kessy ameanza mazoezi ya taratibu ili kurejea kikosini jambo ambalo limeamsha matumaini.
Beki huyo wa zamani wa Simba ambaye kwa sasa anakipiga Yanga, alilazimika kukaa nje baada ya maumivu ya misuli yaliyomfanya ashindwe kuungana na wenzake wakati Stars ikijiandaa kupambana na Rwanda kuwania kucheza Chan.
0 COMMENTS:
Post a Comment