USIKU wa kuamkia leo ilikuwa ni shangwe kwenye Ukumbi wa Mlimani City
wakati wa sherehe ya Rapper nguli wa Bongo ambaye pia ni Mbunge wa
Mikumi Joseph Haule‘Profesa Jay’ aliyefunga ndoa jana hiyohiyo Julai 8, 2017 na mpenzi wake Grace katika Kanisa la St. Joseph lililopo Posta ya Zamani Dar. Katika kusherehekea harusi hiyo, wakati wa kuingia ukumbini Prof. Jay
aliingia akiimba wimbo wake wa ‘Kamili Gado’ huku akiwa amemshikilia
mkewe, Bi. Grace, wimbo ambao uliamsha hisia kwa waalikwa wakiwemo
wabunge Mch. Peter Msigwa na Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambao walionekana
kucheza kwa nguvu zote kumsapoti mbunge mwenzao.
0 COMMENTS:
Post a Comment