July 10, 2017


Uhakika ni kuwa staa wa soka wa England, Wayne Rooney anatarajiwa kutua nchini Tanzania akiwa na kikosi chake cha Everton kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya.

Everton inatarajiwa kucheza mchezo huo ikiwa ni maandalizi kujiandaa na msimu ujao wa 2017/18, ambapo timu hizo zinakutana chini ya udhamini wa SportPesa ambao ndiyo wadhamini wa kuu wa Everton.


Kampuni ya SportPesa iliandaa michuano ya SportPesa Super Cup iliyofanyika jijini Dar es Salaam na Gor Mahia kuwa bingwa ambapo ndipo watakutana na Everton ili kukamilisha michuano hiyo ya mwaka huu, mchezo utachezwa kwenye Uwanja wa Taifa. 

Rooney mwenyewe amesema safari hiyo itamsaidia kujuana vizuri na wachezaji wenzake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic