August 20, 2017



Chuma Suleiman maarufu kama Bi Hindu amesema hana shida na mabadiliko katika klabu ya Simba, lakini atazungumza hadi hapo atakapopata kilichotokea kwenye mkutano maalum wa wanachama wa Simba uliofanyika leo jijini Dar es Salaam na kupitisha mfumo mpya wa uendeshaji.

Wanachama zaidi ya 1200 wa Simba wamekubali klabu yao kuendeshwa kwa mfumo wa hisa huku mmoja pekee akipinga.

Bi Hindu amesema hakuhudhuria mkutano huo kwa kuwa alikuwa katika harakati za kumuozesha mjukuu wake.

“Nilikuwa busy na harusi ya mjukuu wangu na sasa akili yangu ni mechi ya Yanga. Kuhusiana na hilo la mabadiliko sawa tu, nakubaliana. Lakini nitazungumza lolote hadi nitakaposikia kile kilichotokea.

“Kwa sasa nitazungumza nini, sijui waliamua kumpa Mo, au wameamua vingine. Sasa sijui hasa kilichofanyika hapo,” alisema.


Bi Hindu amekuwa kati ya wale waliokuwa wakipinga kufanyika kwa mkutano huo ambao uliitwa mkutano maalum wa wanachama wa Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic