NAHODHA wa
zamani wa Liverpool, Steven Gerrard, amemweleza kiungo wa timu hiyo Philippe
Coutinho, kama anataka vita basi alamishe kwenda Barcelona.
Barcelona
wameshapeleka ofa mara mbili wakimtaka kiungo huyo raia wa Brazil wakiwa na presha kubwa baada ya Neymar
kuondoka hapo na kujiunga na PSG.
Barca wameshaweka
wazi kuwa mchezaji anayeweza kuziba pengo la Neymar ni Coutinho tu, hivyo
wamekuwa wakipambana sana kuhakikisha wanampata.
“Ni vigumu
kumzuia asiondoke, sana sana wachezaji wanaotoka Amerika ya Kusini ambao mara
nyingi wamekuwa wakisema kuwa ni ndoto yao kucheza Barcelona.
“Lakini nafikiri
Barca wameleta ofa mbili nazo zimekataliwa, nafikiri kama akilazimisha kwenda
atakuwa anategeneza vita kwa kuwa Liverpool hawawezi kumuachia kwa urahisi,”
alisema Gerrard.
0 COMMENTS:
Post a Comment