August 7, 2017


Mshambuliaji Nicolas Agyei leo ametambulishwa rasmi katika klabu yake mpya ya Simba.

Agyei ametambulishwa makao makuu ya klabu ya Simba baada ya kuwasili nchini leo usiku.

Raia huyo wa Ghana amekuwa ndiye mchezaji wa mwisho kujiunga wakati wa usajili.

Msemaji wa Simba, Haji Manara ndiye aliyemtambulisha Agyei mbele ya baadhi ya waandishi wa habari na baadhi ya wanachama wa Simba waliokuwa klabuni hapo.


Pamoja na Mghana huyo, wengine waliotambulishwa klabu hapo ni Haruna Niyonzima, Emmanuel Okwi na wenyeji wawili, Method Mwanjale na Mohamed Hussein Zimbwe.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic