August 8, 2017




Kamati ya Rufaa za Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania pia imetoa matokeo ya rufaa nne ilizosikiliza Jumamosi Agosti 5, 2017 zilizokatwa dhidi ya Kamati ya Uchaguzi katika mchakato wa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya TFF.

kamati hiyo. Majibu hayo, yalitoka Kamati ya Rufaa. Warufani walipinga kuondolewa kwenye mchakato wa uchaguzi.

Waliokata Rufaa ni Fredrick Masolwa ambaye awali hakupitishwa kuwania nafasi ya urais kwa kukosa uzoefu kwa mujibu wa kanuni ya 9 (3) ya kanuni za uchaguzi za TFF. Kamati ya Rufaa ilitupilia mbali hoja hiyo kwa sababu ya rufaa kukosa kigezo cha kutolipia kwa mujibu wa katiba ya TFF.

Mwingine ni Mgombea Ujumbe wa Kamati ya Utendaji Kanda namba 7 (Mikoa ya Mbeya na Iringa), Abdusuphyan Sillah awali hakupitishwa kwa kukosa uzoefu kwa mujibu wa kanuni ya 9 (3) ya kanuni za uchaguzi za TFF.

Rufaa yake ilikuwa na vigezo, lakini ilikosa hoja za uadilifu kwa mujibu wa Kanuni ya 9 (7) kwani mrufani alikosa uadilifu kwa kutoa taarifa za uongo mbele ya kamati.

Kanda namba 11 (Mikoa ya Pwani na Morogoro), Hassan Othuman awali hajapitishwa kwa kukosa uadilifu jambo ambalo alilikatia rufaa Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ya TFF. Hata hivyo, alituma ujumbe mbele ya Kamati ya Rufaa akitangaza kujitoa.


Kanda namba 13 Dar es Salaam: Saleh Abdallah awali hakupitishwa kwa kukosa uzoefu kwa mujibu wa kanuni ya 9 (3) ya kanuni za uchaguzi za TFF. Kamati ilitupilia mbali rufaa yake kwa sababu kwanza hakulipia hivyo kukosa vigezo pia hata mrufani mwenyewe hakutokea kutetea rufaa yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic