September 15, 2017



Beki wa kulia wa Simba, Shomary Kapombe, amepewa programu maalum na benchi la ufundi la timu hiyo, linaloongozwa na Mcameroon, Joseph Omog kwa ajili ya kumrudisha katika hali yake kama zamani.

Kapombe ambaye kwa muda mrefu alikuwa akisumbuliwa na maumivu ya nyonga, kwa sasa amepona na ameanzishiwa program hiyo ya mazoezi ya gym kabla ya kuanza mazoezi ya uwanjani na wenzake.

Daktari wa Simba, Yassin Gembe, amesema: “Ni kweli Kapombe tayari amepona kabisa majeraha yake yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu, lakini tumempa programu maalum ya kumfanya awe fiti zaidi ambapo kwa sasa anafanya mazoezi ya gym chini ya uangalizi maalum.


“Atakapokuwa tayari, ataungana na wenzake katika mazoezi ya kawaida ambapo tunatarajia haitachukua muda mrefu kumaliza programu hiyo.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic