September 28, 2017


RUVU SHOOTING

Kamati ya Bodi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi, iliyoketi hivi karibuni imepitia taarifa mbalimbali ya michezo iliyofanyika ya Ligi Kuu ya Vodacom na Ligi Daraja la Kwanza na kufikia uamuzi ufuatao.

Moja ya maamuzi yaliyofikiwa ni kuhusiana na malalamiko ya Ruvu Shooting kwa Kagera Sugar.

AJENDA 13/MSC/2017- MALALAMIKO YA RUVU SHOOTING
Kamati imetupa malalamiko ya klabu ya Ruvu Shooting dhidi ya Adeyum S. Ahmed kupinga mchezaji huyo kuichezea Kagera Sugar bila kuwa na barua ya kumruhusu (release letter) kutoka klabu ya Stand United.


Malalamiko hayo yametupwa baada ya Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF kueleza kuwa Adeyum ni mchezaji halali wa Kagera Sugar, kwani wakati anasajiliwa na timu hiyo alikuwa mchezaji huru kwa vile mkataba wake na Stand United ulishavunjika, hivyo kutohitaji release letter wakati anajiunga na Kagera Sugar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic