September 27, 2017



Simba wametamba kuwa wako vizuri na wataondoka Ijumaa kwenda Shinyanga kuivaa Stand United.

Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema mambo yanakwenda vizuri katika kambi yao ya Mwanza na watakwenda Shinyanga wakiamini pointi tatu ni halali yao.

“Tunaendelea kujiandaa vizuri sana, tunaamini Stand ni timu bora lakini pointi tatu za Stand ni mali yetu.


“Hivyo tunajiandaa kwenda kupambana na kushinda. Pia tuwashukuru sana wanachama na mashabiki wa Simba wa Mwanza ukarimu na kutupokea vizuri,” alisema Manara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic