Baada ya sare ya mabao 2-2 dhidi ya Mbao FC, Simba imesafiri hadi mjini Tabora ambako inaendelea na maandalizi ya mechi ijayo ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Stand United mjini Shinyanga.
Simba iko mjini Tabora na leo itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya wenyeji wake Milambo FC.
Haji Manara ambaye ni Msemaji wa Simba, amesema mechi hiyo ni sehemu ya maandalizi ya mechi yao ijayo.
“Mechi ya kirafiki na Milambo ni leo, baada ya hapo tutaendelea na maandalizi mengine. Tutarejea kambini kumalizia maandalizi kabla ya kuwavaa Stand,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment