September 20, 2017




Hatimaye wachezaji wa Yanga wamerejea kazini leo na kufanya mazoezi.

Mazoezi hayo ya takribani saa moja yamefanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Chini ya Kocha George Lwandamina, wachezaji hao walifanya mazoezi mepedi kabla ya kuondoka na kurejea makwao.

Jana wachezaji hao waligoma kufanya mazoezi wakidai mishahara yao ya miezi miwili.

Hata hivyo, kabla ya mazoezi wachezaji walifanya kikao cha takribani dakika 17 kabla ya kukubaliana na kuanza mazoezi.

Taarifa zinaeleza, wachezaji bado hawajalipwa na wameahidiwa kuwa suala hilo ndani ya siku mbili tatu litakuwa limefanyiwa kazi na kikubwa wao ni kuendelea na kazi.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic