October 26, 2017


KRC Genk imeendeleza ushindi nchini Ubelgiji baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Club Brugge.

Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta ameendelea kuonyesha uwezo wake wa kufunga baada ya kushindilia msumari wa mwisho.

Samatta amefunga bao la pili katika dakika ya 90 baada ya Ruslan Malinovsky kuwa amefunga bao la kwanza katika dakika ya 43.

Samatta angeweza kufunga bao katika kipindi cha kwanza lakini mpira alioupiga ulipaa juu ya lango.


Muda mwingi Mtanzania huyo alikuwa mwiba mbele ya mabeki wa Club Brugge lakini walikuwa makini kuhakikisha hafungi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic