Inawezekana
Msemaji wa Simba, Haji Manara akaingia matatizoni na Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF) ambalo limetaka ufafanuzi kutokana na kauli zake dhidi ya
waamuzi waliochezesha mechi ya Yanga dhidi ya Simba.
Taarifa zinaeleza,
tayari TFF wamesukuma barua kwenda Simba wakitaka ufafanuzi.
“Kuna barua
imepelekwa kutaka kupata ufafanuzi kwa kuwa zinaonekana ni kauli za
kichochezi,” kililieza chanzo.
Lakini mmoja wa
maofisa wa Simba ameiambia SALEHJEMBE: “Hatujapokea barua yoyote, acha
tuendelee kusubiri tutaona itakavyokuwa.”
Manara anatuhumiwa
kuwashambulia waamuzi waliochezesha mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya bao 1-1 na
Yanga kuonyesha soka safi zaidi ya Simba hasa katika ushambulizi.
Lakini Manara
alilalamika Simba kunyimwa penalti likiwemo lile tukio la Kelvin Yondani
kuunawa mpira wakati akijaribu kuondosha hatari langoni mwake.
0 COMMENTS:
Post a Comment