Unaweza kusema ratiba ya mwanzo ya Ligi ya Mabingwa Afrika si ngumu kwa Yanga.
Shirikisho la Soka Afrika (Caf), limeipangia Yanga kuanza na St Louis ya Shelisheli, timu ambayo hauwezi kusema ni mlima mrefu kwa kwa Yanga.
Ingawa Yanga watapaswa kuwa makini kwa kuwa ni soka na soka la Shelisheli limekuwa likipanda, lakini haiwezi kuwa kazi itakayowashinda wakiamua “lazima” wasonge mbele.
Iwapo Yanga itasonga mbele katika hatua hiyo baada ya kufanya vizuri katika mechi mbili dhidi ya St Loius, inatarajia kukutana na mshindi kati ya El Merreikh ya Sudan au Township Rollers ya Botswana.
Iwapo Yanga itasonga mbele katika hatua hiyo baada ya kufanya vizuri katika mechi mbili dhidi ya St Loius, inatarajia kukutana na mshindi kati ya El Merreikh ya Sudan au Township Rollers ya Botswana.
0 COMMENTS:
Post a Comment