December 13, 2017




Ratiba ya Kombe la Shirikisho Afrika imetoka na Simba imepata bahati yah kupangwa na timu laini au kibonde kutoka Djibouti.


Simba imepangwa kuanza Gendamarie, timu ambayo imekuwa ni moja ya vibonde katika michuano ya Kagame ambayo ni maalum kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.


Pamoja na kuanza na kibonde, Simba itatakiwa kujipanga kwelikweli kama itafanikiwa kusonga mbele katika hatua hiyo.

Hatua inayofuata inaonyesha itakuwa ngumu kwa kuwa Simba ikisonga mbele itakutana na timu ya Zambia au Misri.

El Masry ya Misri itakutana na Green Buffaloes ya Zambia na mshindi wa hapo atakutana na mshindi kati ya Simba dhidi ya Gendamarie.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic