December 12, 2017


Mavituuuz ya Mohamed Salah yanaonekana kuwachanganya matajiri Real Madrid ambao wameweka hadharani kwamba wanamtaka.

Tayari Salah aria wa Misri na mchezaji bora wa BBC, amefunga mabao 18 katika mechi za Ligi Kuu England na Ligi ya Mabingwa Ulaya.


Imeelezwa tayari thamani ya Salah aliyetokea AS Roma imefikia pauni million 39 na Madrid inaonekana inataka kumtwaa na pamoja na kuilipa Liverpool, itamtoa Lukas Vazquez.

Salah anaonekana kuwa ndiyo tegemeo la Liverpool katika ushambulizi kila siku zinavyosonga mbele.

Raia huyo wa Misri amekuwa tegemeo katika uchezaji wa timu, utoaji wa pasi za mabao na wakati mwingine kufunga mwenyewe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic