Justin Kluivert ameiongoza timu yake ya Ajax kushinda kwa mabao 3-1 dhidi ya Willem katika Ligi Kuu ya Uholanzi.
Kluivert ambaye ni mtoto wa nyota wa zamani wa Ajax na Barcelona, Patrick Kluivert ameongoza timu yake kushinda bila ya kuwa na Kocha Mkuu Marcel Keizer na msaidizi wake Dennis Bergkamp ambao walikuwa wanatumikia adhabu.
Kinda huyo, ni kati ya wachezaji wanaowaniwa na Manchester United ikiwa ni sehemu ya kuendelea kupanga kikosi chake.
Mabao mengine ya Ajax katika mchezo huo yalifungwa na Kasper Dolberg na David Neres.
0 COMMENTS:
Post a Comment