Zanzibar iemitwanga Uganda kwa mabao 9-5 katika michuano ya Copa Dar es Salaam inayoendelea katika ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam.
Michuano hiyo ya soka la ufukweni kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na Malawi wakiwa wamealikwa, imekuwa kivutio kikubwa leo.
Uganda walionyesha kujitutumua mwanzoni, hata hivyo kipindi cha pili Zanzibar walifunga mabao ya mfululizo na kuwatuliza vijana hao wa Yoweri Kaguta Museveni.
0 COMMENTS:
Post a Comment