December 26, 2017




Klabu ya Yanga imejipanga mchakato wake wa mabadiliko kwenda kwenye uwekezaji kuwa la nchi nzima kwa maana ya maoni.

Mwenyekiti wa kamati hiyo ya mabadiliko, Alex Mgongolwa amesema watafanya juhudi kubwa kuhakikisha mchakato huo unatoa nafasi kwa Wanayanga wengi na Tanzania nzima kutoa maoni yao.

"Lengo ni kufanya mchakato ulio sahihi kitaalamu lakini kuwapa nafasi Wanayanga Tanzania kote kutoa maoni yao.

"Klabu ya Yanga ni ya wanananchi, tunajitahidi kufanya linalowezekana kufanikisha hilo," alisema.

Tayari Yanga imetangaza hata kama ni uwekezaji lazima kutakuwa na mgawanyo wa asilimia 51 na 49.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic