January 25, 2018




Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imesema upelelezi dhidi ya aliyekuwa Rais wa TFF, Jamal Malinzi na wenzake umekamilika.

Awali Mahakama ya Kisutu ilitaka Malinzi, katibu mkuu wa zamani wa TFF, Mwesigwa Celestine na aliyekuwa mhasibu wa shirikisho hilo kuhojiwa tena na Takukuru.

Hivyo Takukuru imeiambia mahakama hiyo kwamba tayari upelelezi huo katika kesi inayowakabiri Malinzi na wenzake kwa tuhuma za utakatishaji fedha imekamilika.


Malinzi na wenzake wako mahabusu tokea mwaka jana huku kesi hiyo ikiendelea kuunguruma katika mahakama ya Kisutu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic