April 26, 2018



Mjumbe wa Baraza la Wazee wa Yanga, Mzee Ibrahim Akilimali, ameomba wanachama na wapenzi wa klabu hiyo kuendeleza umoja ndani ya timu yao ili iweze kufanya vizuri katika mchezo dhidi ya Simba.

Akilimali ameomba hilo kufanyika zikiwa zimesalia siku tatu pekee kukutana kwa watani hao wa jadi, Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mjumbe Akilimali amesisitiza umoja na mshikamano uwepo kwani ndiyo utakuwa nguzo kuu ya kupata matokeo dhidi ya watani wao wa jadi Simba.

Akizungumza na radio One kupitia kipindi cha Michezo, Spoti leo, Akilimali ameeleza kuwa mechi hiyo ni kubwa, hivyo itahitajika kupambana ili kupata matokeo.

Aidha, Akilimali amesema vijana wao wap kambini na wanaandaa dozi maalum ya Simba watakayopewa Jumapili ya wiki hii.

Mechi hiyo yenye hisia kubwa kwa mashabiki na wadau wa soka kwa ujumla nchini, itapigwa Aprili 29 katika Uwanja wa Taifa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic