KIFARU: SIMBA LAZIMA AFE JUMATATU
Msemaji wa klabu ya mtibwa Sugar, Thobias Kifaru, ameitambia Simba kuwa lazima waimalize katika mchezo ujao wa ligi utakaopigwa Jamhuri Stadium.
Kifaru ametamba kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Singida United uliopigwa Uwanja wa Namfua mjini Singida leo.
Mtibwa itakuwa inacheza na Simba katika Uwanja wake wa nyumbani Jumatatu ya Aprili 9 2018 kuanzi saa 10 kamili jioni.
Tayari Simba walishawasili mjini Morogoro kwa ajili ya mchezo huo wakitokea Iringa leo ambapo waliweka kambi maalum kuendeleza mawindo dhidi ya wakata miwa hao.
0 COMMENTS:
Post a Comment