Na George Mganga
Katika mchezo uliopigwa mjini Singida, Mtibwa Sugar imeiadhibu vikali Singida United kwa jumla ya mabao 3-0.
Wafungaji wa mabao hayo ni Kelvin Sabato 22', Salum Kawimbwi 53' na Hassan Dilunga 71'.
Kipingo hicho kinakuwa kuwa ni salaam kwa Simba ambapo Mtibwa watakuwa wanacheza nayo Jumatatu ya Aprili 9 2018 kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Mtibwa wataanza safari yao kurejea Morogoro kesho tayari kuwakabili Simba siku ya tarehe Aprili 9 2018.
Mbali na mechi hiyo, Mbao FC waliokuwa wenyeji pia jijini Mwanza wamelazimishwa sare ya 0-0 dhidi ya Lipuli FC ya Iringa.
0 COMMENTS:
Post a Comment