April 4, 2018



Kocha Mkuu wa Njombe Mji FC, Ally Bushir, ametaja sababu iliyopelekea kupoteza mchezo wa jana dhidi ya Simba.

Bushir ameeleza Simba walikuwa wana uzoefu mkubwa zaidi yao kutokana na aina ya wachezaji walionao tofauti na kikosi chao kilivyo.

Akizungumza mapema baada ya mchezo kumalizika, Bushir alisema Simba ina kikosi kipana huku akimtaja Nahodha wa timu John Bocco namna alivyopata nafasi na kupachika mabao hayo mawili.

"Simba ina wachezaji wenye uzoefu kuliko sisi, tulipata nafasi za kufunga lakini hatukuweza kuzitumia ipasavyo, na hii ni tofauti na wenzetu Simba waliokuwa vizuri. Ukimtazama mchezaji kama Bocco aliweza kutumia uzoefu wake vizuri Uwanjani" alisema Bushir.

Kipigo hicho kwa Njombe Mji kimezidi kuifanya izidi kujiweka kwenye mazingira hatarishi ya kuendelea kusalia kwenye ligi ambapo mpaka sasa ipo katika nafasi ya 15 kwenye msimamo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic