April 7, 2018



Kocha Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa, leo alilazimika kukaa jukwaani kukitazama kikosi cha Yanga kikipambana katika mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Wolaitta Dicha FC.

Nsajigwa hakuwa na namna ya kukaa kwenye benchi la ufundi kutokana na kutumikia adhabu ya kadi ambayo alipewa wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Township Rollers FC huko Botswana.

Kocha huyo aliungana na wachezaji wake ambao wana adhabu ya kadi mbili za njano, Papy Kabamba, Obrey Chirwa aliyerejea leo kutoka Zambia, Kelvin Yondani pamoja na Said Makapu.

Kukaa jukwaani kwa Sanjigwa pamoja na wachezaji waliokuwa wana kadi mbili za njano, kumeipusha Yanga kupatwa na msala mwingine wa adhabu, ambapo sasa watakuwa huru kutumika kwenye michezo ijayo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic