Everton inayoshiriki Ligi Kuu England imemtangaza kocha wake mpya ambaye ni Marco Silva.
Silva anachukua nafasi ya Kocha mkongwe, Sam Allardyce ambaye alitimuliwa.
Mmiliki wa Everton, Farhad Moshiri aliwahi kumtaka Silva kuchukua nafasi ya Ronald Koeman mara baada ya kuacha kazi.
Hata hivyo ilishindikana na kuamua kumchukua Allardyce ambaye hata hivyo alifanikiwa kuwaokoa wasiteremke daraja.
Silva alikuwa kocha wa Hull City lakini msimu uliopita ndiye alikuwa kocha wa Watford ambayo imemaliza msimu wa Ligi Kuu England ikiwa katika nafasi ya 14.
0 COMMENTS:
Post a Comment