May 4, 2018



Kocha wa zamani wa Yanga, George Lwandamina, rasmi ametambulishwa na uongozi wa Zesco United ya Zambia kuwa Mwalimu Mkuu wa timu hiyo.

Lwandamina alirejea nchini kwao kimyakimya akiiacha Yanga kutokana na madai ya fedha za mishahara ambazo hajalipwa.

Zesco wameamua kumrejesha tena Lwandamina wakiwa na imani kuwa atakisaidia kikosi hicho kufanya vizuri katika mashindano ya ligi na kimataifa.

Lwandamina ametambulishwa jana wakati Yanga ikiwa tayari imeshaanza kazi na Mkongomani mpya, Mwinyi Zahera aliyekuja nchini hivi karibuni kuchukua mikoba yake.

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic