Kampuni ya simu ya Airtel Tanzania kwa kushirikiana na kampuni ya kubashiri ya SportPesa imewazaidia washindi watatu wa promosheni ya wa Amsha Amsha ushinde na Airtel Money.
Washindi hao ni Kiliani Moyo, Venus Malima na Frank Mbwana ambao wameshinda simu za kisasa smartphone Samsung Galaxy.
Washindi hao wameshinda katika droo ya kwanza ya promosheni hiyo ambapo jumla washindi 21 walipatikana.
Mbali ya washindi wa simu ya mkononi, pia kulikuwa na mshindi wa televisheni ambaye ni Mkulima wa Tabora, Charles Peter ambaye pia alizawadiwa king’amuzi cha Star Times.
Washindi wengine ni HiIlary Ngarweze, Grace Nsasi, Juma Juma, Chriphod Bunyinyiga, Venus Lugela, Haji Haruna, Jaffari Nkomee na Sige Fadhil.
Walioshinda jezi ni Faraji Namwanga, Omary Said Kaombe, Moses Lifunga, Maulid Salum, Omary Kirangio, Beno Milinga, Augustine Kasiasto, Elias Mgarula na Karato Joel.
Meneja Uhusiano wa SportPesa Tanzania, Sabrina Msuya aliwaomba Watanzania kutumia fursa ya promosheni hiyo na kucheza mchezo wa kubahatisha na kampuni yao ili washinde zawadi nono.
"Hii ni fursa nzuri kwenu kuhakikisha mnajishindia zawadi hizi. Kikubwa ni kucheza michezo ya kubahatisha na SportPesa na mwisho mnafanikiwa kushinda," alisema.
Sportpesa imekuwa ikiaminika zaidi katika michezo hii ya kubahatisha kutokana na lile shindano la Bajaj ambalo limekuwa gumzo kubwa nchini baada ya watu 100 kutoka sehemu mbalimbali nchini kila mmoja kushinda Bajaj aina ya TVS King.
Sabrina alisema kuwa kutumia kampuni yao na Airtel, watanzania wanafursa kubwa ya kujishindia zawadi hizo ambazo zinaweza kubadili maisha yao.
Naye Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando alisema kuwa bado wana zawadi nyingi ambazo zitatolewa kwa washindi na kuwaomba watu waendelee kucheza ili kushinda.
“Kuna walikuwa hawaamini kuwa kuna zawadi hizi, sasa kwa kuwapa zawadi hawa washindi watatu ni njia pekee ya kuwahakikishia wateja wetu kuwa zoezi limeanza rasmi na kuna nafasi kubwa ya kushinda,” alisema Mmbando.
0 COMMENTS:
Post a Comment