Kampuni ya mawasiliano ya imezindua huduma mpya kwa wateja wake wanatuma na kupokea pesa kupitia Airtel Money.
Wateja wa Airtel wanaotumia huduma hiyo kwa sasa wataweza kutuma na kupokea pesa bure kabisa bila makato yoyote.
Akizungumza katika uzinduzi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo nchini, Mkurugenzi wa masoko, Isack Nchunda alisema: “Tuna furaha kubwa kuona ongezeko la watumiaji wa Airtel Money wanaongezeka kila siku, tunaamini kuwa malengo serikali kuhakikisha inafanikisha upatikanaji wa huduma ya kifedha kwa kila mwananchi inalekea kupata mafanikio makubwa.
“Leo Airtel tunazindua huduma hii inayojulikana kama Hakatwi mtu hapa, tuma pesa bure ili kuendelea kuunga mkono juu za serikali na kuwawezesha wateja wetu zaidi ya milioni kumi nchini kuweza kutuma na kupokea pesa bure,” alisema Nchunda.
0 COMMENTS:
Post a Comment