July 5, 2018






Kampuni Star Times imeingia mkataba wa wa kimaudhi na kampuni ya  Trend Solar inayojihusisha na uzalishaji wa Umeme wa Jua kwa kuonyesha matangazo yake kupitia luninga ya kampuni hiyo.

Star Times ambao  kwa sasa wanaonyesha michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Urusi imepewa jukumu hilo la kutoa huduma ya matangazo kwa njia ya kidigitali kutokana na na kuwa na watumiaji wengi barani Afrika ikiwa ni zaidi ya milioni kumi.

 Akizungumza na katika uzinduzi huo uliofanyika jana jijini Dar na kuhudhuriwa na Balozi wa Uingereza nchi, Saraha Crooke, Mtendaji Mkuu wa Star Times, Walker Wang alisema kuwa kushirikiana na Trend Solar ni hatua ya msingi  kwa kuwa kampuni yake inawafikia watu wengi walioko vijijini hasa wale ambao wamekuwa hawapati umeme.

Kushirikiana  na Trend Solar ni hatua ya msingi kwani Star Times tutawafikia watu wengi walioko vijijini  hasa wale ambao hawapato umeme wa gridi, tunayo furaha kubwa kushirikiana  na timu hii katika mradi huu mkubwa wa luninga za kidigitali ili kuwapatia fursa Watanzania wengi zaidi kufurahia maudhui na vipindi vyetu wakiwa na familia zao,” alisema Wang.


 Kwa upande wa  Mtendaji mkuu wa Trend Solar, Irfan Mirza  ambaye ndiyo mwanzilishi alisema kuwa: “Kupitia Trend Solar tunawaondolea watu wetu tatizo la  kusahaulika kwenye maendeleo ya kidigitali kwa kuwapatia Simu ya gharama nafuu.

"Intaneti ya bure na vifaa vya kuchajia nyumbani kutokana na umeme huu ambao hautumi gridi za taifa kwa kupitia mpango huu wa kisasa wa umeme ambao utasaidia jamii kubwa ya Afrika.”
  

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic