July 5, 2018


Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anatathmini ofa kwa kiungo wa kati wa Stoke Xherdan Shaqiri. Mchezaji huyo wa miaka 26 raia wa uswizi anaweza kuondoka Stoke kwa pauni milioni 12. (Sun)

Argentina wanataka meneja wa Manchester City Pep Guardiola kuwa meneja wao mpya kufuatia kutimuliwa kwao mapema kutoka Komb la Dunia.(AS, via Manchester Evening News)

Kiungo mpya wa safu ya kati wa Liverpool Fabinho anasema hakukaribia kujiunga na Manchester United. Mchezaji huyo wa miaka 24 raia wa Brazil alihamia Anfield kutoka Monaco mwezi Mei. (FourFourTwo)

Jack Wilshere amefanya mazungumzo ya ana kwa ana na meneja wa West Ham Manuel Pellegrini kuhusu uwezekano wa kuhamia huko London. Mchezaji huyo wa miaka 26 kiungo wa kati wa England yuko huru baada ya kuondoka Arsenal mwezi uliopita. (Mail)

Meneja mpya wa Arsenal Unai Emery anataka kuwauza wachezaji ili kumsaini kiungo wa kati raia wa Ureno Andre Gomes, 24. (Independent)

Manchester City wanamfuatilia kiungo wa kati wa Melbourne City raia wa Australia Daniel Arzani. Mchezaji huo wa miaka 19 alichaguliwa mchezaji bora wa mwaka nchini Australia na anatajwa kuwa Harry Kewell wa siku za usoni. (Manchester Evening News)

Everton wamefanya mawasiliano na Barcelona kuhusu uwezekano wa kuwepo makubaliano kwa mlinzi wa Colombia Yerrt Mina, 23. (Liverpool Echo)

Kutoka BBC

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic