July 4, 2018


Juventus wana uhakika kuwa watamsaini mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo.

Mchezaji huyo wa umri wa miaka 33 ambaye ni nahodha wa Ureno yuko tayari kukubali mkataba wa pauni milioni 26 kwa mwaka. (Mirror)

Manchester City wako tayari kumsaini wing'a wa Leicester City raia wa Algeria Riyad Mahrez, 27, na kiungo wa kati raia wa Italia Jorginho, 26, kutoka Napoli kwa jumla ya pauni milioni 108. (Mirror)

Chelsea wanataka pauni milioni 70 kwa wing'a raia wa Brazil William wakati Barcelona na Manchester United wanamwinda mchezaji huyo wa umri wa miaka 29. (Mundo Deportivo)

Chelsea wamekataa ofa ya zaidi ya puani milioni 50 kwa William kutoka Barcelona. (Sky Sports)

Tottenham wanataka kumsaini kiungo wa kati mfaransa wa umri wa miaka 23 Adrien Rabiot, kutoka Paris St-Germain. (France Football)

Meneja wa Arsenal Unai Emery anataka kumsaini kiungo wa kati wa Barcelona Andre Gomes msimu huu. Mabingwa hao wa Uhispania wanataka pauni milioni 30 kwa mchezaji huyo wa kimataifa raia wa Ureno. (Independent)

Kiungo wa kati wa Seveilla raia wa Ufaransa Steven N'Zonzi, 29, amekiambia klabu kuwa anataka kuondoka wakati Arsenal inaonyesha nia ya kumsaini. (Sun)

Mshambuliaji wa Chelsea raia wa Uhispania Alvaro Morata, 25, anaweza kutumiwa katika makubaliano ya kubadilishana wachezaji na mshambuliaji raia wa Argentina Gonzalo Higuain 30, kutoka Juventus. (Gazetta dello Sport - in Italian)

Kutoka BBC

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic